Kutwa kwenye usaili

 

TANGAZO KUBWA LA USAILI AJIRA 2026: Serikali Yaita Maelfu ya Waombaji Kwenye Usaili Kuanzia Mei hadi Julai

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma yatangaza ratiba rasmi ya usaili kwa kada mbalimbali Tanzania Bara.

Tangazo la Usaili Ajira 2026

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya taasisi mbalimbali za Serikali ametangaza rasmi majina ya waombaji walioitwa kwenye usaili wa ajira kwa kada tofauti nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa tangazo hilo lililotolewa tarehe 08 Mei 2026, usaili unatarajiwa kuanza rasmi kuanzia tarehe 16 Mei 2026 hadi 25 Julai 2026, huku baadhi ya usaili ukifanyika kwa njia ya mtandao (Online) na mingine kufanyika katika vituo mbalimbali vya usaili nchini.

Taasisi Zilizotangaza Usaili

  • Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC)
  • Shirika la Posta Tanzania (TPC)
  • Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (MOHA)
  • Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC)
  • Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC)
  • Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA)
  • Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
  • Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI)
  • MDAs & LGAs
  • Na taasisi nyingine nyingi za Serikali.

Baadhi ya Kada Zilizotangazwa

ICT Officer II
(Database Administration, Frontend, Backend, Mobile, Security)
Marketing Officer II
(Marketing & Business Development)
Driver II
(TAA, ORCI, MOHA, OSHA, TaSUBa)
Research Assistant & Research Officer
Office Management Secretary II
Investigation Officer II
GIS Officer & Land Surveyor
Economist, Accountant & Finance Officers

Mambo Muhimu kwa Wasailiwa

  • Msailiwa lazima afike akiwa na kitambulisho halali.
  • Vyeti vyote vya elimu vinapaswa kuwa halisi (Original Certificates).
  • Testimonials, Result Slips na Provisional Results havitaruhusiwa.
  • Wasailiwa waliomaliza nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU, NACTVET au NECTA.
  • Kila msailiwa atajigharamia chakula, usafiri na malazi.
  • Kwa usaili wa mtandao, hakikisha unakumbuka email na password ya Ajira Portal.
  • Majina yanayotofautiana kwenye nyaraka yahitaji Deed Poll iliyosajiliwa.

Usaili Wengi Kufanyika Online

Kwa mujibu wa ratiba rasmi, kada nyingi hasa zinazohusiana na Teknolojia ya Habari (ICT) zitafanya usaili wa mchujo kwa njia ya mtandao (Online).

Waombaji wanashauriwa kuingia mara kwa mara kwenye akaunti zao za Ajira Portal ili kuona taarifa za vituo vya usaili pamoja na namba zao za usaili.

ONYO: Serikali imekumbusha kuwa ni marufuku kutoa au kupokea rushwa katika mchakato wa ajira. Ajira zote zinatolewa kwa misingi ya haki, uwazi na sifa stahiki za mwombaji.

PAKUA PDF YA MAJINA NA RATIBA KAMILI YA USAILI

PAKUA PDF

Chanzo: Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) | Tangazo Rasmi la Usaili Mei 2026

Previous Post Next Post