Ajira Mpya: Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi 2026
Kumb.Na.HA.331/388/01/04
Tarehe: 04/05/2026
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi ametangaza nafasi za ajira kwa Watanzania wenye sifa stahiki. Nafasi zilizotolewa ni 2 za Mwandishi Mwendesha Ofisi.
Majukumu ya Kazi
- Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri.
- Kupokea wageni na kuwasaili shida zao.
- Kutunza kumbukumbu za miadi, vikao na safari za Mkuu wa Idara.
- Kutafuta na kusambaza majalada kwa maofisa husika.
- Kukusanya na kurejesha nyaraka sehemu husika.
- Kuandaa dondoo na maandalizi ya vikao.
- Kuandaa mahitaji ya vifaa vya ofisi.
- Kufanya kazi nyingine zitakazopangwa na Mkuu wa kazi.
Sifa za Mwombaji
- Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha Nne (Form IV) au Kidato cha Sita (Form VI).
- Stashahada (Diploma ya Uhazili) au cheti cha NTA level 6 ya Uhazili.
- Uwezo wa kuchapa Kiswahili na Kiingereza maneno 100 kwa dakika.
- Ujuzi wa programu za kompyuta: Word, Excel, PowerPoint, Internet, E-mail na Publisher.
Ngazi ya Mshahara
TGS C
Masharti ya Jumla
- Raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18–45.
- Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kuomba.
- Kuambatanisha CV yenye maelezo binafsi, anuani, simu na referees watatu.
- Vyeti vya elimu na taaluma lazima vithibitishwe na Mwanasheria/Wakili.
- Vyeti vya nje ya nchi lazima vihakikiwe na TCU, NECTA au NACTE.
- Waombaji waliostaafu hawaruhusiwi bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
- Maombi ya kughushi yatapelekea hatua za kisheria.
- Mwisho wa kutuma maombi: 19/05/2026.
Jinsi ya Kuomba
Waombaji wanapaswa kuwasilisha barua ya maombi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu kwa anuani:
Mkurugenzi Mtendaji (W),
Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi,
S. L. P 18,
MALINYI.
Maombi yote yatumwe kupitia mfumo wa kielektroniki wa Ajira kupitia Recruitment Portal.
Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu hayatazingatiwa.
