Tangazo la Kuitwa Kazini - Mei 2026
Ofisi ya Rais - Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
Maelezo Muhimu
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwataarifu waombaji kazi waliofanya usaili kati ya 24 Mei 2025 na 14 Februari 2026 kuwa matokeo ya waliofaulu yameorodheshwa rasmi.
Waombaji wote waliofaulu na kupangiwa vituo vya kazi watazipata barua zao kupitia akaunti zao za Ajira Portal (sehemu ya My Applications). Wana wajibu wa kupakua na kuchapisha barua hizo na kuripoti katika vituo walivyopangiwa.
Wakifika vituoni, wanatakiwa kuwasilisha vyeti halisi vya masomo kuanzia kidato cha nne ili vihakikiwe kabla ya kupewa barua ya ajira.
Kwa majina ambayo hayapo kwenye tangazo hili, tafadhali fahamu kuwa haukufaulu na unaweza kuomba tena nafasi nyingine zitakapotangazwa.
Pakua Tangazo Kamili
Ili kuona orodha kamili ya majina na vituo vya kazi, tafadhali pakua tangazo rasmi kwa kubofya kiungo hapa chini:
